Monday, October 22, 2012

apa marehemu Oming'o alikuwa anafuatilia kwa karibu mpambano uliokuwa ukipigwa kati ya Segerea na Mburahati Veterans.
Jacob Aridi - Oming'o (aliyejishika kiunoni) alikuwa ni shabiki nambari moja wa Simba na Liverpool, hapa ilikuwa ni ktk mpambano wa mashabiki wa simba na wale wa Yanga.. siku zote palikuwa panachimbika. tutakukosa mno kamanda na rafiki wa kweli. Pumziko la Amani ulipate na raha milele utapewa na mwanga wa milele utaangaziwa.
Marehemu Jacob Odhiambo Aridi- Oming'o alikuwa daima ni mcheshi na mtu alokuwa mstari wa mbele kulisogeza mbele gurudumu la segerea veterans, hapa ilikuwa ni mitaa ya mburahati. Pumzika kwa Amani
TANZIA
Wana Segerea Veterans and Social Club wanasikitika kutangaza kifo cha mchezaji mwenzetu, Jacob Othiambo Aridi, al-maaruf kama Oming'o ( aliyeruka juu akiwa na jezi ya barcelona) kilichotokea akiwa anafanja mechi mazoezi pamoja na timu za Moro United na Segerea Veterans siku ya jumamosi tarehe 19/10/2012 saa 2.30 asubuhi katika uwanja wa Toto Tundu Segerea, juhudi zote za kunususru maisha ya marehemu Oming'o zilifanyika lakini mapenzi ya Mungu yaheshimiwe. Mwili wa marehemu Oming'o utaagwa nyumbani kwake Segerea Sanene siku ya jumanne tarehe 23/10/2012 kuanzia saa 9.00 alasiri na kusafirishwa kesho yake kuelekea Rorya Mara kwa mazishi. TUTAKUKUMBUKA DAIMA.

Thursday, April 12, 2012

Ghettob Prez, nyemo Chinyabe na mbwiga wa mbwiguke, pombe zilitawala ukumbini 2000 kigogo

wanasoka mahiri wa zamani nchi hii wakimsikiliza mpiga soga za soka kutoka kushoto ni Mao Mkami "Ball Dancer" Mbwiga wa Mbiguke, Dua Bin Said na Spear Mbwembwe wakijiuliza nini kinatokea kwa wachezaji wa siku hizi kila siku kubadili mitindo ya nywele na kiwango cha soka kinaporomoka tu



Nyemo John Chinyabe, Salum Mwamtuya na Paul Kidubo wakiangalia swag za mbwiga wa mbwiguke hapo mjini kigogo 2000
Msafiri Mohameid na kiongozi mwanzilishi wa Kigogo veterans wakitafakari jambo


Omar Tamba kiongozi wa friends veterans na mchezaji mahiri wa timu ya Simba SC. akimkabidhi Mh: Ally Katembo Mwenyekiti wa Segerea Veterans zawadi ya pasaka kwa niaba ya timu mbili hizo siku ya jumamosi 7/4/2012 katika ukumbi wa 2000 kigogo

mlinzi mahili wa timu za vijana (kabaka yeka) na simba za dar es salaam Omar Tamba ambaye pia ni kiongozi wa Timu ya Friends Veterans akiwa katika mazungumzo na shabiki namba moja wa segerea veterans Sweety

kiongozi shupavu wa soka kinondoni Msafiri Mohameid alikuwa mgeni wa heshima katika hafla ya kigogo veterans siku ya jumamosi ya pasaka 2012 katika ukumbi wa 2000

spear mbwembwe, mao mkami ball dancer, mbwiga wa mbwiguke na dua said kabla akijaanza kupigwa kiwanjani

Bakar Idd "Beka Joo" akikaguliwa kabla ya mechi na segerea veterans na kigogo veterans siku ya jumamosi ya pasaka segerea veterans ilishinda 3-0